Wednesday, September 28, 2016

Miaka 80 ya Simba Sports Club nilikuwepo uwanjani

Nilikuwepo uwanjani pamoja na mashabiki lukuki wa Simba nikimshuhudia mnyama akimrarua AFC Leopards ya Kenya mabao 4-0 kwenye uwanja wa Taifa, Jijini Dar Es Salaam. Wote tukiimba kila mtu 'Mavugooo'. Mchezaji huyu wa Kimataifa kutoka Burundi,  Laudit Mavugo alitupia bao katika mechi yake ya kwanza akiichezea SSC. Ilikuwa raha sana. Nimeweka kumbukumbu ya kuhudhuria mechi ndani ya uwanja wa Taifa wakati Simba inatimiza miaka 80 tangu ianzishwe.

No comments: