Thursday, September 15, 2016

Tuangalie ugonjwa wa nyanya kuoza kitako (Blossom endrot)


Baadhi ya wakulima wa nyanya wamekuwa wakipata tatizo la nyanya zao kuungua chini ya kitako na kuharibu kabisa ubora wa nyanya hizo. Wanataalamu wanatueleza kuwa ugonjwa huo unaitwa kuoza kitako (Blossom endrot). Hii husababishwa na mmea kukosa maji ya kutosha au kutofuata ratiba ya umwagiliaji kwa zao hilo.Unakuta siku nyingine unamwagilia asubuhi siku nyingine mchana au unamwagilia Jumamosi halafu unarudia tena kumwagilia siku ya Jumanne huko ndiko kutozingatia ratiba ya umwagiliaji. Hiki ndicho chanzo kikuu cha ugonjwa huo wa kuoza kitako.
 
 TIBA

Ondoa matunda yote yaliyo athirika halafu anza kufuata na kuzingatia ratiba ya umwagiliaji wa shamba lako.
(Hii nimeinyaka kutoka fb wafanyakazi wa kilimo Mifugo na uvuvi na kuikarabati kidogo na kuirusha kwani ni wengi wanalima nyanya na hasa na kuwaona wanamwagilia maji kiubabaishaji tu).

No comments: