Thursday, September 15, 2016

Unapoitaja Matombo unagusa matunda na machenza

Machungwa na machenza ya Matombo, Morogoro ni matamu sana. Tatizo wafanyabiashara wameingilia kati biashara hii na kuyauza machenza na machungwa wakati bado hayajafikia kukomaa kibailojia (Yanakomaa yakiwa mtini). Kibaya zaidi huchanganya machungwa au machenza mazuri na mabaya. Mlaji akibahatika hula chenza tamu na ikiwa hana bahati unaweza kula chenza chungu. Hii ni kuharibu biashara na umaarufu wa machungwa au machenza ya nyumbani Matombo. Kwa kawaida machungwa huanza kuvunwa kuanzia mwezi machi hadi Juni.

No comments: