Friday, November 27, 2015

Brass Band kichochezi cha kuanza shule mapema

Nilipokuwa mdogo nilivutiwa sana na Brass Band. Shule ya Msingi Matombo ilkuwa na vifaa vizuri sana vya band kama unavyoviona  kwenye hiyo Brass Band ya Polisi. Ingawa nilikuwa mdogo na mfupi lakini nilitamani kupiga ngoma ndogo,kubwa na pia kuwa Bandmaster  (huyo aliyeshika gongo). Hii ndiyo moja ya sababu iliyonifanya kuanza shule mapema. Na kweli nilipoingia shule nikiwa darasa la nne tu niliweza kuwa mpiga ngoma ndogo, nikiwa darasa la sita ngoma kubwa (huku nikibebewa) na hatimaye Band master (ingawa gongo lilikuwa zito na wakati mwingine kushindwa kuzungusha kwa manjonjo).

Magufuli ofisini kwa Majaliwa-Hapa Kazi Tu


Jana tarehe 26 Novemba, Mhe. Rais Dkt.John Joseph Pombe  Magufuli alimtembelea Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa ofisini kwake. Hapa Kazi Tu!

DC Josephine wa Shinyanga akuta dawa kibao kituo cha Afya Kambarage

Katika ziara ya ghafla aliyoifanya DC Josephine  Matiro kwenye kituo cha afya cha Kambarage. Yeye pamoja na Katibu Tawala wa Wialya (Pichani) walipigwa butwaa kukuta dawa zimejaa kibao huku wagonjwa wakiambiwa hakuna dawa hivyo wajinunulie wenyewe.chukua ni kumsimamisha kazi mmoja wa wauguzi wa zahanati hiyo (Picha kwa hisani ya Mahunde blog)

Watu tumeumbwa tofauti

Wakati Mhe.Diwani Nicholaus Kampa wa Kata ya Vikindu alipowaalika wapiga kura wake na kuwashukuru, huyu (alikuwa amelewa) alichukua chakula kiasi hiki. Kwa kuwa nilikuwepo kwenye hafla hii, nilimshuhudia akichukua chakula mara mbili. Kweli watu tumeumbwa tofauti.

Hii ndiyo Lyamungo Guest House-Moro

Moja ya Guest Houses nzuri zinazopatikana mjini Morogoro- Lyamungo Guest House. Siipigii debe, lakini kwa kweli Guest hii ni nzuri, safi na usalama wa hali ya juu. Kinachofurahisha zaidi ni uchapa kazi wa watoa huduma wa nyumba hii ya wageni wakiongozwa na Meneja wao Bw. Malamsha. Bei ya chumba kwa siku ni Tshs 25,000/=  inajitegemea na chenye kiyoyozi. Ipo karibu kabisa na "msikiti wa Mahita"

Friday, November 20, 2015

Wengi hatupendi kuandika na wala kusoma


Ukitaka kuwa na ufahamu wa kutosha katika maeneo mengi ni lazima ujifunze kusoma na ikiwezekana na kuandika pia. Ukitaka kuwa mtafiti mahiri lazima usome na kuandika. Pichani ni baadhi ya  taarifa mbalimbali na Thesis za  MSc na PhD zinazotunzwa kwenye maktaba ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika-Idara ya Utafiti na Maendeleo.

Maembe yanavyooza kiwanda cha Azam

Hivi ndivyo inavyoonekana kwa moja ya lori lililobeba shehena ya maembe nje ya kiwanda cha Azam (Bakharesa Group) likingoja zamu ya kuuza maembe hayo. Maembe mengi yamekuwa yakioza nje ya kiwanda hicho kwa sababu ya mchakato wa muda mrefu ya kuyanunua kiwandani. Aidha usafirishaji wa maembe hayo ni wa kiholela sana. Ona jinsi yalivyojazwa kwenye viroba na kufungwa na kamba. Kwa vyovyote uwezekano wa kuharibika ni mkubwa sana.Wasafirishaji wanatakiwa  kuelimishwa kuhusu hili.

Hawana wasiwasi

Hawana wasiwasi na usalama wao wanajua watafika salama tu. Je, hujawahi kuina hii hapa Dar?

Macho kwa macho na Simba

    Ingekuwa wewe ungefanyaje?

Atafika salama tu

Hii inaitwa kuhama poa. Umetumia chombo cha usafiri cha uwezo wake. Ili mradi kimesafirisha kilicho chake kutoka pointi A kwenda B. Atafika salama tu

Nadhani lori litakuwa limebeba madini

Hadi kufungwa kwa kamba. Nadhani bidhaa hiyo ni madini yenye thamani!

Unakaribishwa kununua petrol

Hivi bango hili lilikuwa lina maana ya ice cold cocacola au Petrol. Kwa kweli nimeshindwa kuelewa. Tuwe makini katika kuandika mabango.

Nadhani askari wa barabarani watakuwa wamelala

Hana wasiwasi imejiamini japokuwa ni hatari. Wako wapi askari wa barabarani?

Nini hicho kwenye keki ya mifugo?

Inakuwaje? Hivi machine ndiyo iliyofunga  keki hii ya mifugo?

Hahahaa when maize is used to pay school fees

Nchi inapotumia mahindi kulipia karo (ada) ya shule basi uchumi wake ni hoi bin taabani!

Imekosewa au?

Hata kama hujui kiingereza hizo zilimo ndani ya gari ni njugu kweli?

Mtafiti Dr. Peter Massawe

Dr. Peter Massawe .Mtafiti kiongozi wa zao la korosho nchini akiwasilisha mada katika mkutano wa kimataifa wa zao la korosho uliofanyika  jijini Dar Es Salaam mwezi huu.

Dereva anapokuletea 30,000/=

Haijalishi gari lako linabeba mzigo gani lakini kwa kuwa mmepatana kwa siku ni shilingi 30,000/=. Hivi ndivyo gari lako linavyoumia na dereva kufaidika

Tuesday, November 17, 2015

Jengo la Mikutano Morogoro -EDEMA

Hili ni jengo la Mikutano liitwalo EDEMA lililoko mjini Morogoro, karibu kabisa na Chuo Kikuu cha Kiislam (Zamani  Chuo cha TANESCO) - Morogoro maeneo ya Msamvu.

Madiwani wa Jimbo la Mkuranga

Madiwani wapya wa Jimbo la Mkuranga wakiwa na Mbunge Mhe.Ulega. Wakwanza kulia ni Mhe. Nicholaus Kampa, Diwani wa Kata ya Vikindu.Aliyevaa suti nyeusi ni Mwenyekiti wa CCM-Mkuranga.

Mavuno ngazi ya Jumuiya-Parokia ya Viklndu




Wanajumuiya ya Mt. Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Vikindu (Mt. Vinsenti wa Paulo) Jimbo Kuu la Dar Es Salaam wakiwa katika maadhimisho ya Siku ya mavuno ngazi ya Jumuiya tarehe 31/10/2015. Kiasi ch shilingi 1,000,000/= kilikusanywa kupitia michango na mnada uliyofanywa na Jumuiya.

Mhe. Ulega Mbunge wa jimbo la Mkuranga

Huyu ndiye Mbunge wetu wa Mkuranga. Mhe.Ulega

Wednesday, November 4, 2015

Natunukiwa cheti cha Advanced Management

Napata cheti change baada ya kuhudhuria mafunzo ya Advanced Project Management chuoni Mananga, Swaziland  mwezi  Agosti 2015