Wednesday, December 15, 2010

Sangara wameadimika ziwani Victoria


Mwaka 1985 nilibahatika kuhudhuria mafunzo ya muda mfupi ya Rural Comminication kwenye chuo kilichojulikana Nyegezi Social pale Mwanza sasa hivi St. Agustino University. Siku moja tulipangiwa kusafiri na meli ya Chuo Cha Uvuvi iliyojulikana kama MV-Mdiria. Tulitumia siku nzima kuvua samaki kwenye ziwa Victoria. Tulivua samaki wengi sana wakubwa kwa wadogo. Samaki aina ya Sangara wakati huo walikuwa wengi na wakubwa lakini hawakuwa na soko. Nakumbuka baada ya safari ili ya kichuo kwa madhumuni ya kuandika habari tulipewa Sangara mkubwa mmoja ili tugaweane na sisi tulikuwepo watano tu. Hivi sasa Sangara ni adimu ziwani victoria wamevualiwa sana na kusafirishwa nchi za nje (mapande)sasa bei ya samaki haikamatiki jijini Mwanza.Hapa ndipo tulipofikia.

Saturday, December 4, 2010

Dr. Fidelis Myaka- Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo


Dkt Fidelis A.Myaka ndiye Mkurugenzi mpya wa Idara ya Utafiti na Maendeleo katika Wizara ya Kilimo chakula na Ushirika kuanzia Januari 2010. Anashahada ya uzamivu katika nyanja ya agronomia.

Katika utumishi wake wa umma hasa utafiti ameshughilikia sana utafiti wa mazao jamii ya mikunde (mbazi,kunde,choroko) na kuongoza programu za utafiti katika kanda kama kiungo wa habari na mawasiliano katika kanda, mratibu wa utafiti katika kanda pamoja na kukaimu nafasi ya Mkurugenzi wa Utafiti kanda ya Mashariki kuanzia mwaka 2008 hadi mwanzoni mwa mwaka 2010.

Anayo machapisho ya kitaalamu yapatayo 40 na amewahi kunyakua tuzo ya kwanza ya uchapishaji katika katika mashindano yaliyoandaliwa na Idara mwaka 2006. Elimu yake ya msingi ameipata katika shule zilizoko katika mikoa ya Kagera na Pwani. Sekondari 'O'level Pugu Sekondari na 'A' level Mkwawa Sekondari. Alirushwa kutoka shahada ya Kwanza hadi Uzamivu. Waswahili au hata wachaga huita'Kichwa.'

Anapendelea sana masuala ya TEKNOHAMA.

Dr.Kafiriti na mamaa


Muda wa sherehe za kuagwa wastaafu. Dr. Elly Kafiriti - Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti wa Kilimo kanda ya Kusini alikuwa makini kabisa kwenye meza yake pamoja na mkewe. Kanda hiyo iliwazawadia vifurushi vya korosho wastaafu wote pamoja na viongozi wapya wa Idara wa lioteuliwa akiwemo Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo Dkt. Fidelis Myaka.

Champaigne kwa waagwa


Kinywaji kwa wanaoagwa kwanza.

Nilifungua champaigne


Kama sikosei hii ni champaigne yangu ya nne kuifungua katika tafrija mbalimbali. Kizibo kilirushwa juu kabisa. Naanza kuwa mtaalamu.

Wazee wa EAAPP


Wageni waalikwa walikuwa ni wengi kutoka vituoni na makao makuu pia hata wazee wa EAAPP (Rice Centre of Excellence) walikuwepo.

Tunywe kwa afya zetu



Unapokuwa na furaha unakunywa na kula na ndugu zako, marafiki zako, wafanyakazi wenzako na wengine. Ndivyo wanavyosema wastaafu waandamizi wa Idara ya Utafiti na Maendeleo walioagwa hivi karibuni.

Familia ya Chambi


Wengi huwa wanauliza hivi pale Kibaha unafanyika utafiti wa miwa hivi wanafanyaje? Swali hilo ni rahisi kwa Mzee Juhudi Chambi. Ingawa amestaafu lakini kutokana na maarifa, utaalamu na uzoefu katika utafiti wa miwa swali hili ni rahisi kwa Mzee Chambi. Muda wake mwingi katika utumishi wa umma ametumikia katika utafiti wa miwa pale Kibaha akiwa mratibu wa utafiti wa zao hilo pamoja na uongoziwa Kituo cha Utafiti wa Miwa-Kibaha. Mzee Chambi ni mtu wa QUALITY kama alivyosimulia mwenyekiti wa Sherehe za kuwaaga wastaafu Bw. Ninatubu Lema. Ni mtaalamu wa uzalishaji wa mazao (Plant Breeder). Ni mkarimu sana na mcheshi ni mtu wa familia kama anavyoonekana pichani akiwa na familia yake katika tafrija ya kumuaga iliyoandaliwa na Wizara tarehe 19 Novemba 2010. Juhudi zake katika zao la miwa ni kuongeza uzalishaji wa zao la miwa bora kwa kutatua tatizo la mbegu bora zenye kuvumilia magonjwa na wadudu.

Timothy Kirway

Kwa wafanyakazi wa Wizara ya Kilimo jina la Kirway si geni. Kwanini? Kirway aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi Utafiti wa Mifumo ya Kilimo na Uchumi Jamii kama ilivyo kwa wafanyakazi waliozaliwa mwaka wa 1950 alistaafu rasmi katika utumishi wa umma mapema mwaka huu. Mzee Kirway atakumbukwa zaidi kwa kuchapa kazi na umakini wa kazi na hasa ufuatiliaji na utunzaji wa kumbukumbu. Daima alisimamia haki na usawa. Ndiye hasa mwanzilishi wa utafiti shirikishi na mifumo ya kilimo hapa nchini.Pichani katika kumbukumbu ya kuagwa kwake akiwa na mkewe katika viwanja vya KILIMO II tarehe 19/11/2010.

Dr. Shomari Shamte mstaafu wa Kanda ya Kusini


Aliyekuwa Mkurugenzi wa Utafiti kanda ya Kusini,Dr. Shamte Shomari amestaafu kazi kwa mujibu wa sheria katika mwaka wa fedha 2009/10. Dr. Shomari atakumbukwa zaidi katika utendaji kazi wake kwa umma kwa zaidi ya miaka 30 katika kuboresha utafiti wa korosho hapa nchini. Ndiye Mkurugenzi mwanzilishi wa kanda ya kusini na pia ameboresha kwa kiasi kikubwa mazingira ya kazi katika kituo cha Utafiti wa Kilimo-Naliendele. Tarehe 19 Novemba 2010 Wizara iliandaa tafrija ya kuwaaga wastaafu waandamizi akiwemo Dr. Shomari. Pichani Dr. Shomari akiwa ametulia tuli na mkewe.

Watafiti waandamizi wastaafu waagwa

Tarehe 19 Novemba 2010. Idara ya Utafiti na Maendeleo iliyoko katika Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika iliwaaga wastafu waandamizi kwa mwaka 2009/10. Tafrija hiyo ya nguvu ilifanyika kwenye viwanja vya makao makuu ya wizara KILIMO II. Walioagwa ni Dr. Mohamed Msabaha (Pichani akiwa na mkewe)aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi - Utafiti wa mazao, Bw. Timothy Kirway aliyekuwa Mkurugenzi wa Utafiti Mifumo ya Kilimo na Uchumi Jamii, Dr. Shamte Shomari aliyekuwa Mkurugenzi wa Kanda wa Utafiti- Kusini, Dr. Ally Mbwana aliyekuwa Mkurugenzi wa Kanda wa Utafiti-Kaskazini na Bw. Juhudi Chambi, Afisa Mfawidhi kituo cha Utafiti wa Miwa na Mratibu wa Utafiti wa Miwa -Kibaha. Dr. Msabaha atakumbukwa zaidi katika ubunifu wake wa kukifanya kituo cha Uyole kuwa mfano wa kuigwa katika uzalishaji wa mbegu za mazao hasa mahindi na maharagwe. Aidha katika utendaji kazi wake alisimamia ubora wa kazi na kuvumiliana.

Sunday, November 28, 2010

Tunaposhindwa kujitosheleza kwa umeme

Ili nchi iweze kuendelea, nishati ya umeme ni lazima ipewe kipaumbele. Nchi nyingi nilizowahi kutembelea hasa Ulaya. Suala la kukosa umeme hata kwa dakika tano tu halijawahi kutokea. Hapa nyumbani ukatikaji wa umeme ni kitu cha kawaida kabisa. Umeme unaweza kukatika hata kwa miezi mitatu na bado kusiwe na uhakika wa kupatikana. Kibaya ni pale ambapo tunapopata maelezo yanayobadilika kila kukicha kutoka kwa mamlaka husika. Leo, Transformer ya Kipawa imeharibika, kesho mtambo wa Songas umeshindwa kuzalisha umeme. Keshokutwa IPTL imekosa mafuta ya kuendesha mitambo, mtondogoo kina cha maji Kidatu kimeshuka. Tatizo ni nini hasa? Kwa kukosa umeme uzalishaji katika sekta zote huathirika. Siyo wakati wa kuweka mkakati. Tunahitaji umeme wa uhakika.

Dar inaoza!

Jana katika pitapita zangu maeneo ya Kariakoo hasa mtaa wa Msimbazi nilikuta uchafu wa kutisha. Mitaro imeziba na maji machafu yalikuwa ya kitiririka.Ni balaa kabisa. Kama unatembea na viatu vya wazi ni rahisi kabisa kugusa maji hayo machafu na yanukayo.

Tatizo nilionalo ambalo ni kiini cha uchafu uliokithiri jijini ni watu wenyewe. Mitaro imezibwa kwa chupa za maji takataka za mazao mabalimbali na mifuko ya plastiki.

Jambo jingine ni kwamba jiji halina utaratibu mzuri wa kuliweka jiji katika hali ya usafi.Hivi kuna mabwana afya wa jiji kweli. Ah, jamani inabidi kulinda afya za wananchi, aidha jiji lazima livutie kwa usafi. Tujizatiti sote kuiweka DAR ssfi.

Monday, November 22, 2010

Hawa ndiyo wabunge wako


Huu ndiyo mtazamo wa bunge jipya!

Hatujamuelewa Papa kuhusu matumizi ya Kondom


Baba Mtakatifu Benedict xvi hajahalalisha matumizi ya kondom kama wengi wanavyodai. Alichosema pale inapobidi ili kuokoa UHAI Kondom inaweza kutumika. Inabidi tutafakari kwa kina vinginevyo tunaweza kupotosha.

Utamu wa pweza uonje!


Zamani nilikuwa sili pweza lakini siku hizi nikiwaona tu wamekaangwa na kuwekwa mezani pale Buguruni au Mbagala sikosi kuonja kipande kimoja au viwili. Kuna vipande vinavyouzwa sh.100/= (kidogo) na kikubwa sh. 200/=. Ukitaka kumfaidi pweza lazima uweke chachandu. Angalia bakuli la chachandu pichani.

Alipohutubia walitoka



Wakati Rais Jakaya Kikwete alipolihutubia Bunge jipya kwa mara ya kwanza Novemba mwaka huu. Wabunge wa CHADEMA walitoka ukumbini. Kisa? Hawamtambui RAIS. Hivi muswada ukipitishwa Bungeni mtu wa mwisho kusaini ni nani?

Thursday, November 4, 2010

What are the signs of high blood Pressure?

How do you know if you have it or not?
The bad news is that in most cases you simply can't tell-high blood pressure, or hypertension, usually has no symptoms that you can detect.

Hypertension is called "the silent killer" because with time, untreated, it can lead to a variety of health problems, and does so without you noticing anything.

High blood pressure can lead to increased heart size, aneursyms, kidney failure and arthelescerosis, where your arteries become damaged - and other serious health problems. (cont...)

Blood Pressure

Wasomaji wangu, leo nimeona niwaletee hii makala bila ya kuitafsiri kwani ni ya maana sana kwa maisha yetu.

What is Blood Pressure?

Blood pressure is the measure of how much pressure your blood puts against the various blood vessels of your body. It is important because if it is too high, your body, and especially your heart, will slowly start to become damaged.

The damage this causes takes a lot of time to happen but can be very serious-it can lead to issues like coronary artery disease, stroke and kidney damage, among other things.

Heart disease is a single worst killer of people in many parts of the world. (cont....)

Zawadi kutoka kwa Wazazi


Wazazi wa Eric walikuwa wa kwanza kutoa zawadi. Wao walimvisha Rosari!

Mjomba hakosi zawadi


Ningekuwa Matombo ningepeleka kuku au mbuzi na mke wangu asingekosa kikapo cha mpunga. Kwa kuwa shughuli hii ilifanyika katika mazingira ya kileo tena mjini Morogoro zawadi yangu ilikuwa ni hii. Msiniulize kilichomo ndani ya box!

Wednesday, November 3, 2010

Tukishatoa zwadi tunapongeza wazazi


Ni kawaida yetu tukishatoa zawadi tunawapongeza watu muhimu kama vile wazazi.Pichani Baba mkubwa wa Eric Prof.Moshi akimpongeza mama Eric. Hongera shemeji!

Prof. Moshi kanisani Kigurunyembe

Haitoshi tu kuserebuka. Inatupasa kuhuduria ibada pia.

Monday, November 1, 2010

Kutunza na kutunzwa


Wazazi walitunzwa na Amina alitunzwa. Ndivyo ilivyokuwa siku ya Send Off ya Amina usiku wa tarehe 23/10/2010 katika ukumbi wa VETA - Mikumi.

Ulikuwa mwezi wa shughuli


Tulianza kwa kumwaga Joyce Kyando Luhungu. Baadaye Ushemasi wa tarehe 23/10/2010Jakka Oscar wa Morogoro.Jioni kule Mikumi Send-Off ya Amina Omary Jakka. Kesho yake 24/10/2010- Morogoro, Komunio ya kwanza ya Eric Mkoba. Watu ni wale wale ilibidi wengine wagawane kwani kote kulituhusu. Lakini kuna wale waliobahatika kuhudhuria shughuli zote tatu Mungu awabariki. Pichani Amina Jakka(kulia) akiwa na mmewe kwenye Send-Off ya Mikumi.

Saturday, October 30, 2010

Tatizo Kuosha vyombo


Shughuli ni nzuri lakini tatizo ni pale shughuli inapokwisha na sasa inabidi vyombo vioshwe. Kasheshe!

Hata Moro ipo 'Kiduku'

Vijana wa Moro walitupatia show ya 'Kiduku'

Bia bwelele


Huwezi kuamini, kulikuwa hakuna kadi ya kuingia ukumbini lakini wageni walikula na kunywa. Hakika bia zilikuwa bweleleee!

Bro Omari Jakka wa Mikumi alikuwepo


Tuliondoka Mikumi saa 12 asubuhi kuelekea Morogoro kwa nia ya kushuhudia Komunio ya Kwanza ya Eric. Pichani Bro Omari Jakka wa Mikumi na Dada Irene Banzi wakilisakata ruhmba ukumbini Tushikamane.

Dogo Elvis naye alikuwepo


Kama kuna mwalikwa ambaye alifurahi sana wakati wa sherehe za kumpongeza Eric Mkoba pale Tushikamane-Morogoro basi ni Elvis G.Banzi (Pichani)

Mama alirushwa juu juu


Ndugu, marafiki na majamaa walimrusha juu kwa juu Mama Eric (Restituta) huku wakimpongeza kwa zawadi mbalimbali hasa khanga na vitenge.

Wakati wa kuburudika


Baada ya kushughulika sana wajomba mama mkubwa wanaburudika. Pichani kutoka kushoto Gaitan Banzi,Anthony Kunambi, Faustini Mizambwa na Mama Mkbwa Dr.Doreen Moshi wakiburudika kwa raha zao! kwenye tafrija ya kumpongeza Eric ukumbini Tushikamane-Kilakala, mjini Morogoro.

Wengi walilishwa Keki




Eric aliwalisha keki wazazi, ndugu na marafiki zake waliohudhuria sherehe hiyo.

ERIC ALIKATA KEKI YA KOMUNIO YA KWANZA

Kabla ya kupata chakula Eric alikata Keki ya Komunio ya Kwanza.

Friday, October 29, 2010

Wamekuja kumpongeza

Ndugu, jamaa na marafiki kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini walikuja kushuhudia na kumpongeza Eric Mkoba kwa kupata Komunio ya Kwanza.

Thursday, October 28, 2010

Safari imeanza


Baada ya kumaliza Ibada, safari lianza kurudi nyumbani ambako Eric alipokelewa kwa shangwe na vigelegele.

Kanisa la Kigurunyembe


Kanisa hili lipo kwenye eneo kilipo Chuo cha Ualimu Kigurunyembe. Chuo hiki kina historia muhimu ya nchi hii inayohusu Elimu. Walimu wengi wamepitia chuoni hapa. Kilichonishangaza kwenye chuo hiki ni uchakavu wa miundo mbinu yake. Licha ya kujengwa mahali pazuri na plan nzuri. Miundombinu ni chakavu kwelikweli. Kwa wale wanaoifahamu Kigurunyembe ya wakati huo walisikitika kuona kuwa chuo kimekwisha. Kuna haja ya kuanza kukikarabati chuo hicho na kurudia enzi zake za zamani.

Eric Mkoba amepata Komunio


Kwa Mkristo Mkatoliki Sakaramenti ya Komunio ni moja ya sakaramenti 7 muhimu katika kanisa hilo. Jumapili iliyopita Eric Mkoba wa Kilakala Morogoro alipata Komunio ya Kwanza kwenye Parokiani Kigurunyembe, Mkoani Morogoro baadaye tafrija ya nguvu ilifanyika katika ukumbi wa TUSHIKAMANE.

Friday, October 22, 2010

Kariakoo ni kila kitu


Ukitaka kununua kitu chochote jijini Dar Es Salaam, tembelea maduka yaliyopo Kariakoo. Hapa hakuna kinachokosekana. Pichani mteja anafanya kinachoitwa 'window shopping'

Wataalamu wa kilimo wajadili habari za udongo


Hivi karibuni wataalamu wa kilimo wapatao 15 wengi wakiwa ni watafiti walikutana jijini Dar Es Salaam kupata taarifa ya Mradi wa Afsis wenye lengo la kukusanya na kusambaza taarifa za udongo barani Afrika zitakazorahisisha kutoa maamuzi sahihi ya matumizi ya udongo katika kilimo ili kuongeza tija na kuongeza kipato cha wakulima.

Paroko wa Vikindu Fr.Tommy

Paroko wa Parokia ya Vikindu Fr. Tommy (pichani kushoto)akitoa maelekezo wakati wa utoaji wa sakramenti ya Kipaimara iliyotolewa tarehe 17/10/2010 hapo parokiani.

Mjue Askofu Libena


Askofu Salutaris Melchior Libena alizaliwa tarehe 23 Nov 1963 Itete,Mahenge,mkoani Morogoro, alipata daraja la upadri tarehe 29 June 1991 akiwa na umri wa miaka 27. Mwaka 2010 Januari, 28 aliteuliwa kuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo la Dar es Salaam, Tanzania na alisimikwa rasmi daraja la Uaskofu tarehe 19/3/2010 ni mmoja kati ya Maaskofu vijana, Tanzania.

Thursday, October 21, 2010

Mwenyekiti wa Parokia alitoa Shukrani


Mwenyekiti wa Parokia ya Mt.Vincent wa Paulo, Vikindu alitoa shukrani kwa niaba ya waumini kwa Askofu Salutaris Libena kwa kufika Parokiani kwa mara ya kwanza na kutoa Sakramenti ya Kipaimara kwa waumini.

Walijipanga kumshika mkono Askofu Salutaris


Waumini wote wakiwemo masista baada ya misa walijipanga kumshika mkono Askofu Libena

Parokia ya Vikindu ilifurika


Jumapili ya tarehe 17/10/2010 iliandika historia nyingine kwa parokia ya Vikindu. Kanisa lilifurika kama inavyoonekana pichani.

Askofu Salutaris atoa Kipaimara Vikindu


Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki,Jimbo Kuu la Dar Es Salamu Mhashamu Askofu Salutaris Melchior Libena Jumapili ya tarehe 17/10/2010 alitoa sakramenti ya Kipaimara kwa waumini 75 katika Kanisa Katoliki Mt.Vincent wa Paulo,Parokia ya Vikindu. Libena aliwataka waumini hao kuishi Kikristu. Alitoa onyo kwa wale wanaosahau sakramenti ya Kitubio na kuwataka kuwa wakatoliki hai kwa kushiriki Ibada zinazoendeshwa na Kanisa.

Naongea na Dr. Assenga


Siku ya Chakula Duniani nilipata bahati ya kuongea na Dr. Assenga, DALDO wa Ilala.

Walijionea wenyewe


Mambo ya Kimbiji yalikuwa makubwa, wajasiriamali kutoka Halamashauri za Wilaya za Temeke, Ilala na Kinondoni walileta bidhaa mbalimbali za vyakula vilivyoongezwa samaki. Hata sambusa zilipatikana hapohapo!

Tulifika Kimbiji


Baada ya kusafiri umbali wa zaidi ya kilomita 60 hatimaye tulifika Kimbiji na kushiriki kwenye maonyesho ya Siku ya Chakula Duniani Kitaifa.