Saturday, December 4, 2010

Dr. Shomari Shamte mstaafu wa Kanda ya Kusini


Aliyekuwa Mkurugenzi wa Utafiti kanda ya Kusini,Dr. Shamte Shomari amestaafu kazi kwa mujibu wa sheria katika mwaka wa fedha 2009/10. Dr. Shomari atakumbukwa zaidi katika utendaji kazi wake kwa umma kwa zaidi ya miaka 30 katika kuboresha utafiti wa korosho hapa nchini. Ndiye Mkurugenzi mwanzilishi wa kanda ya kusini na pia ameboresha kwa kiasi kikubwa mazingira ya kazi katika kituo cha Utafiti wa Kilimo-Naliendele. Tarehe 19 Novemba 2010 Wizara iliandaa tafrija ya kuwaaga wastaafu waandamizi akiwemo Dr. Shomari. Pichani Dr. Shomari akiwa ametulia tuli na mkewe.

No comments: