Saturday, December 4, 2010

Familia ya Chambi


Wengi huwa wanauliza hivi pale Kibaha unafanyika utafiti wa miwa hivi wanafanyaje? Swali hilo ni rahisi kwa Mzee Juhudi Chambi. Ingawa amestaafu lakini kutokana na maarifa, utaalamu na uzoefu katika utafiti wa miwa swali hili ni rahisi kwa Mzee Chambi. Muda wake mwingi katika utumishi wa umma ametumikia katika utafiti wa miwa pale Kibaha akiwa mratibu wa utafiti wa zao hilo pamoja na uongoziwa Kituo cha Utafiti wa Miwa-Kibaha. Mzee Chambi ni mtu wa QUALITY kama alivyosimulia mwenyekiti wa Sherehe za kuwaaga wastaafu Bw. Ninatubu Lema. Ni mtaalamu wa uzalishaji wa mazao (Plant Breeder). Ni mkarimu sana na mcheshi ni mtu wa familia kama anavyoonekana pichani akiwa na familia yake katika tafrija ya kumuaga iliyoandaliwa na Wizara tarehe 19 Novemba 2010. Juhudi zake katika zao la miwa ni kuongeza uzalishaji wa zao la miwa bora kwa kutatua tatizo la mbegu bora zenye kuvumilia magonjwa na wadudu.

No comments: