Wednesday, December 15, 2010

Sangara wameadimika ziwani Victoria


Mwaka 1985 nilibahatika kuhudhuria mafunzo ya muda mfupi ya Rural Comminication kwenye chuo kilichojulikana Nyegezi Social pale Mwanza sasa hivi St. Agustino University. Siku moja tulipangiwa kusafiri na meli ya Chuo Cha Uvuvi iliyojulikana kama MV-Mdiria. Tulitumia siku nzima kuvua samaki kwenye ziwa Victoria. Tulivua samaki wengi sana wakubwa kwa wadogo. Samaki aina ya Sangara wakati huo walikuwa wengi na wakubwa lakini hawakuwa na soko. Nakumbuka baada ya safari ili ya kichuo kwa madhumuni ya kuandika habari tulipewa Sangara mkubwa mmoja ili tugaweane na sisi tulikuwepo watano tu. Hivi sasa Sangara ni adimu ziwani victoria wamevualiwa sana na kusafirishwa nchi za nje (mapande)sasa bei ya samaki haikamatiki jijini Mwanza.Hapa ndipo tulipofikia.

No comments: