Saturday, December 4, 2010

Watafiti waandamizi wastaafu waagwa

Tarehe 19 Novemba 2010. Idara ya Utafiti na Maendeleo iliyoko katika Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika iliwaaga wastafu waandamizi kwa mwaka 2009/10. Tafrija hiyo ya nguvu ilifanyika kwenye viwanja vya makao makuu ya wizara KILIMO II. Walioagwa ni Dr. Mohamed Msabaha (Pichani akiwa na mkewe)aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi - Utafiti wa mazao, Bw. Timothy Kirway aliyekuwa Mkurugenzi wa Utafiti Mifumo ya Kilimo na Uchumi Jamii, Dr. Shamte Shomari aliyekuwa Mkurugenzi wa Kanda wa Utafiti- Kusini, Dr. Ally Mbwana aliyekuwa Mkurugenzi wa Kanda wa Utafiti-Kaskazini na Bw. Juhudi Chambi, Afisa Mfawidhi kituo cha Utafiti wa Miwa na Mratibu wa Utafiti wa Miwa -Kibaha. Dr. Msabaha atakumbukwa zaidi katika ubunifu wake wa kukifanya kituo cha Uyole kuwa mfano wa kuigwa katika uzalishaji wa mbegu za mazao hasa mahindi na maharagwe. Aidha katika utendaji kazi wake alisimamia ubora wa kazi na kuvumiliana.

No comments: