Saturday, December 4, 2010

Dr. Fidelis Myaka- Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo


Dkt Fidelis A.Myaka ndiye Mkurugenzi mpya wa Idara ya Utafiti na Maendeleo katika Wizara ya Kilimo chakula na Ushirika kuanzia Januari 2010. Anashahada ya uzamivu katika nyanja ya agronomia.

Katika utumishi wake wa umma hasa utafiti ameshughilikia sana utafiti wa mazao jamii ya mikunde (mbazi,kunde,choroko) na kuongoza programu za utafiti katika kanda kama kiungo wa habari na mawasiliano katika kanda, mratibu wa utafiti katika kanda pamoja na kukaimu nafasi ya Mkurugenzi wa Utafiti kanda ya Mashariki kuanzia mwaka 2008 hadi mwanzoni mwa mwaka 2010.

Anayo machapisho ya kitaalamu yapatayo 40 na amewahi kunyakua tuzo ya kwanza ya uchapishaji katika katika mashindano yaliyoandaliwa na Idara mwaka 2006. Elimu yake ya msingi ameipata katika shule zilizoko katika mikoa ya Kagera na Pwani. Sekondari 'O'level Pugu Sekondari na 'A' level Mkwawa Sekondari. Alirushwa kutoka shahada ya Kwanza hadi Uzamivu. Waswahili au hata wachaga huita'Kichwa.'

Anapendelea sana masuala ya TEKNOHAMA.

2 comments:

chib said...

Kinachosubiriwa ni utendaji tuuu

Anonymous said...

salam kenal dariku
salam blogger indonesia
http://f4dLyfri3nds.blogspot.com