Saturday, February 27, 2016

Sh2-Mdundo bila umeme












Wote hawa wanafurahi mdundo wa ngoma ya Kiluguru iitwayo shilingi 2. Hii ngoma ilitumbuiza siku ya harusi ya Bw na Bibi  Macarios  Banzi. Kikundi hiki ni cha watu sita na kila mmoja hupiga,huimba na kucheza. Kwa kawaida hupiga ngoma kwa muda mrefu na hubadilisha midundo mumo kwa mumo. Unacheza upendavyo. Hiyo ndiyo shilingi 2 mdundo bila umeme wala amplifier!

Asante sana Bw & Bi. Michael Luanda

Bi. M.Luanda akiwaongoza Ex-NJOSS kwenda kutoa zawadi kwa Bw & Bi Macarios Kushoto Michael Luanda na katikati Mr.Lawrence Mkude. Asante sana kwa Big Support. Udumu urafiki na undugu wetu.

Harusi ya Macarios Banzi- Watu walicheza sana









Harusi ya Macarios- Kila mmoja aliyekuwa ukumbuni alicheza jinsi alivyogusa kuna wale waliogswa na ngoma ya asili ya shilingi 2 kuna sisi vijana wazamani tulioguswa na old is gold na vijana walicheza bongo flava na kwaito. Woo kwa kweli hapakukalika. Hebu check picha ya chini kabisa mimi mambatsa mu moko pamoja na Mr.Mkude tukiyarudi magoma!

Welldone Brother

Baada ya kazi ngumu ya maandalizi, dogo Omari ananipongeza. Asante sana dogo nadhani siku ile ya harusi wewe ulilala tarehe 7/2/2016!

Meza moja na marafiki zangu wa Tosamaganga


Picha ya Juu. Tangu mwaka 1978 hadi leo, kutoka Tosamaganga hadi Dar  miaka zaidi ya 36 sasa. Banzi, George Mnyitafu (Ngi) na Chris Kalanje (aliyevalia miwani) kushoto kwake Mrs.George. Walisafiri hadi Vikindu kunipa tough na kumpongeza dogo Macarios kwa kufunga ndoa. . Pembeni yao na marafiki wapya maisha mapya Vikindu. Asanteni sana.

Mr. Lawrence Mkude

Kaka yangu na mmoja wa marafiki zangu  wa muda mrefu - Matombo, Nombe Sekondari, Manzese-Dar hadi hii leo. Nilipo upo. Asante sana.

Hawa ni ndugu zetu upande wa MAMA















Harusi ya Bw. Macarios Banzi na Martina ilivuta watu wengi. Hapa ni baadhi ya ndugu zake (zetu) upande wa mama yetu walioabahatika  kuhudhuria shamrashamara hizo pale Tandan - Vikindu. Hakika ni Bahati ya pekee.

Hawa ndiyo ndugu zetu upande wa BABA

Shangazi Paulina Kibena a.k.a Mama Mloka
































Nilipta fursa ya kuwatambulisha ndugu zetu upande wa baba kwa kuzingatia mama waliozaa baba na shangazi zetu. Hawa ni baadhi tu waliohudhuria sherehe za harusi ya Bw. Macarios Banzi na mkewe Martina siku ya tarehe 6/2/2016.