Monday, October 27, 2014

Ndege aina ya Kwale

Ndege aina ya Kwale. Hivi Kwale ni  Kiingereza au Kiswahili- Wataalamu wa lugha mpo?

Eti una gari

Hivi hii ni gari au store ya kuhifadhi ndizi ziive?

Bw. Remmy anataka mtoto wa Kike


Bw. Remmy Shayo ulipofika wakati wa kulisha keki watoto yeye alimchagua mtoto wa kike akitaka awe wa kwanza kupatikana katika ndoa yao.

Furaha tupu

Eti harusi imefana sana mwenzangu. Bw & Bibi  Kijimbo wakifurahia jambo ndani ya ukumbi wa Maaskofu, Kurasini jijini Dar wakati wa tafrija ya mapokezi ya Bw & Bibi Remmy shayo tarehe 26/10/2014

Watoto waliruhusiwa

Mapokezi ya Bw & Bi Remmy Shayo yameonyesha upendo mkubwa kwa watoto,waliruhusiwa na kuhudumiwa sawa na wakubwa

Iko siku nao watafunga ndoa

Watoto wasindikiza maharusi wakiingia ndani ya ukumbi wa Maaskofu-Kurasini, jijini raha wakati wa sherehe ya kuwapongeza Bw & Bibi Remmy Shayo wa Vikindu, Mkuranga kwa tendo la kufunga ndoa.

Bw & Bibi Remmy Shayo








Bw na Bibi Remmy Shayo ndani ya Ukumbi wa Maaskofu -Kurasini, jijini Dar wakati wa tafrija fupi ya kuwapongeza baada ya kufunga ndoa siku ya tarehe 26/10/2014

Wageni waalikwa-Harusi ya Remmy Shayo



Mapokezi ya Bw & Bibi harusi Remmy Shayo wa Vikindu, Mkuranga- Wageni waalikwa wakiwa ndani ya ukumbi wa Maaskofu Kurasini jijini Dar- 26/10/2014

Ujana raha tupu!





Unamuona huyo mwenye fulana ya kijani. Kijana anapenda muziki huyo acha tu. Alitupa burudani ya aina yake jana kwenye ukumbi wa Maaskofu-Kurasini jijini Dar. Enzi zangu miaka ya 80s nilikuwa kama yeye. W-end niko Silversands Hotel na kaka yangu Lawrence Mkude nikisakata Disco la nguvu. Ah nikwambie nini ujana raha tupu!

Ulifika wakati kwa Bw. Remmy kupeleka keki ukweni



Mara nyingi kwenye sherehe za kuwapongeza maharusi kuna tendo la kupeleka keki kwa wakwe. Hii maana yake nini hasa. Kwa ufahamu wangu ni ishara ya ukarimu na kuwa tayari kujitoa na hasa chakula. Wakwe wanahitaji kutunzwa na kuwakarimu. Tuwakarimu wakwe na ndugu na watu wengine. Pichani Bw. Remmy akikabidhi keki ukweni siku ya sherehe ya harusi yake - 26/10/2014

Bw & Bibi Remmy Shayo katika matukio tofauti





Madada wasindikiza harusi kutoka Mwandege








Kikosi hiki cha madada wasindikiza harusi kutoka Mwandege, Mkuranga. Mama mwanakamati wa maandalizi ya sherehe ya harusi ya Remmy Shayo alijitolea kukileta kikundi hiki ili kipendezeshe mapokezi ya harusi hiyo iliyofanyika jana (26/10/2014). Kwa kweli walikonga nyoyo za waalikwa. Walicheza kwa furaha na walikuwa very simple! Kweli Mungu yu Mwema.

Mc- Tegete akifanya vitu vyake ndani ya ukumbi wa Maaskofu- Kurasini

MC-Tegete ni mmoja kati ya maarufu wanaochipukia jijini Dar. Hapa anaonyesha vitu vyake ndani ya ukumbi wa Maaskofu  Kurasini wakati wa sherehe  ya harusi ya Bw na Bibi Remmy Shayo wa Vikindu-Muranga (26/10/2014)

Harusi ya Remmy ilivyofana kwenye Ukumbi wa Maaskofu Kurasini-Dar








Bw & Bibi Remmy Shayo wa Vikindu- Dar Es Salaam jana tarehe 26/10/2014 walifunga ndoa kwenye Kanisa la TAG Vikindu na baadaye tafrija ya Nguvu ilifanyika ndani ya Ukumbi wa Maaskofu Kurasini. Hakukuwa na kinywaji chochote cha kilevi lakini watu walifurahi na kuserebuka kama unavyowaona pichani. Banzi wa Moro alikuwa ndani ya ukumbi.

'Mtumishi wa Mungu' George - Zunguka zunguka


Saturday, October 25, 2014

Misa ya Mavuno Jumuiya ya Mt. Vincent Parokia ya Vikindu - 25/10/2014





Leo 25/10/2014 asubuhi, Padri Jinu wa Parokia ya Vikindu aliendesha  ibada ya misa takatifu ya mavuno iliyodhinishwa kwenye Jumuiya  ya Mt. Vincent. Kwenye mahubiri yake alisema kuwa, mara nyingi binadamu tunamsahau MUNGU. Tunapofanikiwa katika maisha yetu tunafikiri ni kwa sababu ya akili zetu au juhudi zetu binafsi. MUNGU TUNAMUWEKA KANDO. Tujiulize katika maisha yetu, hivi hatuna chochote cha kumwambia MUNGU ASANTE? Na hii ndiyo maana ya MAVUNO ni kutoa SHUKRANI KWA MUNGU. Tumsifu YESU KRISTU.