Tuesday, January 4, 2011

Mwaka 2011 wa changamoto

Nimeuanza mwaka 2011 kwa changamoto nyingi. Kubwa zaidi ni kwamba mwaka 2010 haukuisha vizuri kwa upande wa mawasiliano. Nina matatizo makubwa kimtandao hivyo kushindwa kuwasiliAna nanyi hadi mwaka huu ulipokwisha.

Tatizo jingine ni kukatika kwa umeme mara kwa mara. Hata hivyo leo nimejitahidi kuweza kupata fursa ya kuweza kurusha hii ya kwanza kavukavu. Ni kweli mwaka 2011 umeanza na changamoto nyingi. Lakini nyingi ni zile zile. Hivi kweli Watanzania tunashindwa kutatua matatizo yetu hata yale ambayo ni mepesi tu. Tusiwe wavivu kiasi hicho. Mwaka 2011 uwe wa kuchapa kazi zaidi kupambana na changamoto zinazotukabili.

Nawashukuru sana wasomaji wangu wa Banzi wa Moro. Big up kwa wale waliokuwa wanaochangia mada hasa Mwana IT - BELO!

HERI YA MWAKA MPYA

No comments: