Tuesday, January 4, 2011

Hivi ni halali kweli magari ya mafuta kutumia Kilwa Road

Amini usiamini kuna mlolongo wa magari makubwa yanayotokea Kigamboni na kupitia barabara ya Kilwa yakitokea Kongowe hivyo kusababisha msongamano wa magari kuanzia Mbagala Rangi Tatu hadi Kizuiani. Aidha, barabara hiyo haikujengwa kwa kupitisha magari yenye uzito mkubwa. Tutegemee nini hivi karibuni?

Barabara itaanza kuwa na mabonde na milima na hatimaye kushindwa kupitika. Mipango yetu na matumizi vioane. Tujiulize, hivi ni nani aliyeruhusu kujengwa visima vya mafuta ukivuka Kigamboni?

No comments: