Thursday, January 20, 2011

WanaTosa wakutana Peacock


Wataalamu na wafanya biashara 12 waliosoma Tosamaganga High School miaka ya mwisho ya 70 walikutana jijini katika Hotel ya Peacock kwa lengo la kumpongeza mwanatosa mwenzao Dr.Haji Mponda kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii.
Aidha walitumia fursa hiyo kumpongeza pia Dr.Florence Turuka ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu Wizara ya Sayansi na Teknolojia.

Wanatosa hao walimweleza bayana Waziri huyo kuwa wanajivunia kuona kuwa TOSA imetoa zao ambalo limeonekana kufaa kuongoza katika moja ya sekta muhimu nchini (AFYA). Walimsihi Waziri kuhakikisha kuwa anaacha 'legacy' katika Wizara hiyo. Waziri aliwawakikishishia wanaTosa kuwa hatowaangusha na yupo tayari kupokea ushauri utakaomsaidia kufanya kazi yake kwa ufasaha zaidi. Pichani G.Mnyitafu (NGI) mmoja wa waratibu wa shughuli akizungumza kwa niaba ya wanatosa katikati ni Waziri Mponda na Kushoto ni Dr.Turuka.

No comments: