Thursday, January 20, 2011

Hicho kikombe cha kijani ni cha nini?


Kwa sisi tunaojua kula mafenesi. Hicho kikombe cha kijani kimwekwa mafuta ya kula. Kwa kuwa mafenesi yana utomvu hivyo ukitaka kula fenesi kwanza ni vyema ukachovya vidole vyako kwenye mafuta kwa kufanya hivyo utomvu hautoganda vidole na hivyo kufaidi fenesi (local knowledge). Mafenesi kama haya kutoka Morogoro ni matamu sana lakini hayana bei. Hebu fikiria fenesi moja huuzwa kwa bei ya shilingi 1000 na 2500 kweli inalipa?

No comments: