Wednesday, January 26, 2011

Noti mpya tena!

Jana katika pitapita zangu mitaani nilifika pale Tahfif kupata mahitaji ya clear packets (mifuko ya kutunzia maandiko nakusomeka-tafsiri yangu). Pale nilimkuta mama mmoja naye akipata mahitaji yake. Mhudumu wa duka alipomrudishia 'change' akampa na noti mpya na kumtahadharisha kuwa ikidondokea maji tu basi itakuwa imeshaharibika. Kusikia hivyo yule mama akairudisha ile noti mpya. Mimi nikashangaa kusikia hilo na sikuamini. Baadaye mchana wakati nakula chakula cha mchana nikasikia habari hiyohiyo kuwa noti mpya ubora wake ni wa hali ya chini ukilinganisha na noti za zamani. Hivi ni kweli hapa ndipo tulipofikia? Tatizo la umeme liko nje ya uwezo wetu. Hata kutengeneza noti tumeamua kuwa na noti zinazochuja?

No comments: