Tuesday, January 4, 2011

Watanzania si Wavivu

Jumapili tarehe 2/1/2011 nilimtemebelea mzee wangu Mapunda kule Yombo Dovya. Nikiwa ndani ya daladala niliona wananchi wakishughulika na shughuli mbalimbali. Kuna waliokuwa wakiuza mitumba, kuna akina mama waliokuwa wakiuza korosho za kukaanga,samaki wa kukaanga, wengine walikuwa wakiuza mananasi na maembe.

Nikajiuliza jana mwaka mpya leo jumapili lakini hakuna anayepumzika. Abiria mwenzangu alinijibu anayesema Watanzania wavivu hajui alisemalo. Hivi utalalaje wakati hujui utakula nini? Utastarehe vipi wakati senti mfukoni hakuna?Wanaosema hivyo ni kukejeli wananchi! Watanzania si wavivu wanatakiwa kutengenezewa mazingira mazuri ya kufanya kazi.

No comments: