Thursday, October 21, 2010

Askofu Salutaris atoa Kipaimara Vikindu


Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki,Jimbo Kuu la Dar Es Salamu Mhashamu Askofu Salutaris Melchior Libena Jumapili ya tarehe 17/10/2010 alitoa sakramenti ya Kipaimara kwa waumini 75 katika Kanisa Katoliki Mt.Vincent wa Paulo,Parokia ya Vikindu. Libena aliwataka waumini hao kuishi Kikristu. Alitoa onyo kwa wale wanaosahau sakramenti ya Kitubio na kuwataka kuwa wakatoliki hai kwa kushiriki Ibada zinazoendeshwa na Kanisa.

No comments: