Wednesday, September 14, 2016

Bus la Yutong la Wachina

Hili ni bus la Yutong la kutoka Uchina. Utawapenda tu. Wachina ni wazuri kwa teknolojia.  Hutengeza kuteka matakwa ya mdau. Hapa Tanzania kwa sasa naweza kusema kuwa asilimia 80 ya mabus ni  ya Kichina. Inasemekana ni bei poa ukilinganisha na mabus aina ya Scania au Marcopolo. Kingine wanachofanya  Wachina ni kuongeza thamani ya bidhaa. Ukipanda mabus yao yalivyorembwa na kuwekewa vikorombwezo vingine hakika hutoacha kulipanda tena. Sisi tutaanza lini kuunda mabus yetu?

No comments: