Sunday, September 21, 2008

Samaki uhai wa akina mama wa Mkuranga

Kila siku asubuhi asilimia 40 ya wasafiri kutoka Mkuranga kwenda jijini Dar ni wanawake. Wengi wa wanawake hawa hubeba ndoo za plastiki. Hii inaashiria nini? Ndoo hizo hutumika kubeba samaki wanaowanunua kutoka soka la samaki Kigamboni. Wanawake hawa ni mahili sana. Hujua kukimbilia mabasi, huamka mapema asubuhi na hutunza fedha zao sehemu ambayo itakuwa vigumu kwa vibaka kuiba! Jem biashara ya samaki inalipa? Anajibu mama mmoja. Inalipa baba ikiwa unamtaji mzuri. Pia inategemea soko kule Kigamboni. Kweli akina mama hawa wameweza kufanya mengi kupitia biashara ya samaki kama vile kusomesha watoto. Aidha huwasaidia akina baba kuboresha bajeti ya nyumbani!

No comments: