Wednesday, September 3, 2008

MKULLO KACHEKA KWENYE ATM

Siyo siri mtu wangu, kama zali vile, nilikuwa nimechacha ile mbaya. Hata mwanangu Mary alikuwa analitambua hilo kwani zawadi ilikuwa hakuna tena. Maana si unajua, kama alivyosema bosi wetu wa TUCTA kuwa mshahara ni "mbolea" ya wafanyakazi. Mbolea hiyo ilichelewa kutufikia si ya "kupandia" wala "kukuzia"! Ikawa malumbano kati ya "TUCTA" na Ma Ghasia na Mzee Mkullo wa "Treasury"? Si ndo ikwa ahadi, ahadi na huku "TUCTA" ikisisitiza kuwa kama hiyo mbolea haitatolewa wafanyakazi wataingia barabarani? Basi kama zali mwanangu leo asubuhi kuweka vitu kwenye ATM mbolea waaa!

No comments: