Wednesday, September 3, 2008

LUGALUGA WAANZA KUJITAYARISHA KWA KILIMO

Ushirika wa Kilimo na Maosko ujulikanao kwa jina la Lugaluga lenye makao yake makuu katika Manispaa ya Morogoro hivi sasa imeanza kutayarisha mashamba yao tayari kwa msimu wa kilimo 2008/9. Kwa mujibu wa Katibu wa Ushirika huop Bw. John Waziri. Ushirika huo una eneo la shamba lipatalo ekari 16,000 katika kijiji cha Kimambira wilayani Mvomero.

Ushirika huo wenye wanachama wapatao mia moja umepanga kulima ekari 2000 za mpunga kwa mwaka 2008/9.Tayari mipango ya kuwakopesha matrekta wanachama wa Lugaluga uko kwenye hatua za mwisho. Kupatikana kwa matrekta hayo yasiyopungua matano kutawawezesha washirika hao kutayarisha mashamba yao mapema tofauti ilivyokuwa mwaka jana ambapo matrekta yalichelewa kuanza kazi shambani.

Akiongea na blog hii Bw. John Waziri amesema kuwa wanapata ushirikiano mzuri kutoka kwa viongozi wa ngazi zote mkoani Morogoro wakiwemo Mkuu wa Mkoa Meja Jenerali Saidi Kalembo na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Bi Hawa Ngulume cha kutia moyo ni kwamba wameshatembelea eneo la shamba hilo kubwa.

Blog hii ilipata nafasi ya kufika kimambila na kuona shamba hilo na kushuhudia jinsi wananchama walivyokuwa na ari ya kujikita kwenye uzalishaji wa kilimo.

Mashamba ya Kimambila yakiboreshewa miundo mbinu (hasa barabara za kufika shambani,maji na umeme. Na iwapo wakulima watapata zana za kilimo kama vile matrekta na kupata fursa ya kupata pembejeo za kilimo (mbolea, mbegu na viuatilifu) kwa wakati wakati unaofaa.Kuandaa mtandao wa kilimo cha umwagiliaji. Yanaweza kuzalisha chakula cha kutosha na kuchangia katika adhima ya kuufanya mkoa wa Morogoro kuwa ghala ya chakula ya Taifa.

No comments: