Wednesday, September 24, 2008

ATCL mnatuangusha

Niko jijini Gaborone, Botswana tangu jana kuhudhuria warsha kuhusu Menejimenti ya Habari na Mawasiliano katika Utafiti wa Kilimo na Maendeleo. Safari yangu kufika hapa haikuwa nzuri hata kidogo. Kwanza tulichelewa kuondoka Dar kwa masaa 8. Kwasababu hiyo tuliikosa ndege ya kuunganisha toka Johanesburg kwenda Gaborone. Hata hivyo tulifanikiwa kuunganishwa kwenye ndege ya AIR Botswana. Wakati wote tulipokuwa Dar tukisubiri kuundoka tulikuwa tunatangaziwa kuwa tutaondoka saa 5.30, mara saa 7.30 kitu ambacho hakikutokea hadi tulipoondoka saa 8.30. Abiria wapatao watatu ilibidi wavunje safari zao kwani walijua kuwa wasengeweza kuwahi shughuli zao au kupata ndege ya kuunganisha huko waendeko.

Wazungu wawili (mtu na mkewe) tuliosafiri ndege moja ambao walikuwa ni watalii kutoka Afrika ya Kusini hawakusita kusema kuwa walipokuwa Tanzania mambo yalikuwa mazuri sana walisifu vivutio vyetu vya utalii (Bara na visiwani) ni vizuri sana na kusema Watanzania ni wakarimu sana na ni wa amani. Tatizo ni kwenye usafiri wa ndege kwani wakati wakiwa nchini kulikuwa na uchelelewaji wa ndege kuondoka kila waliposafiri na hasa ATCL. Ndugu zangu ATCL kweli mnatuangusha. Tatizo ninaloliona mimi ni menejimenti kuto kutoa uamuzi sahihi kwa wakati unaofaa. Halafu pale Airport kuna wafanyakazi wengi tu wanazagaa zagaa sijui na wa Swissport kazi yao ni nini?

No comments: