Thursday, September 25, 2008

Nchi za SADC na Upashanaji Habari katika Kilimo

Wataalamu 22 kutoka nchi 14 zilizo katika umoja wa SADC wanaendelea na warsha ya kujadili jinsi ya kutumia nyenzo ya Habari na Mawasiliano katika kuboresha uzalishaji katika Sekta ya Kilimo. Wataalamu hao wanaangalia ni wadau gani wanaohitaji habari za kilimo, wanazitumiaje habari hizo, zinapatikanaje, mikakati gani itumike kuhakikisha kuwa mfumo unakuwepo wa kutumia habari na mawasiliano ili utumike katika kuwasaidia watunga sera na watoa maamuzi katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo katika sekta ya kilimo, ni uwezo gani uliopo kwenye masuala ya habari na mawasiliano kwa wadau wa kilimo. Nyenzo na utaalamu upo? Hayo ndiyo mambo yaliyotuleta hapa Gaborone, Botswana kwa muda wa siku tatu. Tanzania inawakilishwa na wataalamu wawili huku jinsia ikizingatiwa. Wataalamu wanatoa hoja zao za nguvu mambo yanachambuliwa na kuwekwa sawa. Hatimaye viongozi wetu tutawaeleza. Cha ajabu katika kundi hili Afrika ya Kusini hawamo licha ya kuwa wanachama wa SADC. Naambiwa aah wao wameshapiGa hatua kubwa kwenye nyanja hii. Nchi zinazoshiriki katika warsha hii ni Tanzania, Zambia, Malawi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Kongo (DRC),Zimbabwe, Lesotho, Swaziland,Mauritius,Seychelles,Madagascar,Mozambique,Angola,Namibia na wenyeji wetu Botswana.

No comments: