Wednesday, October 8, 2008

Mitihani kuvuja-Lawama kwa wazazi,wamiliki shule

Kuanzia Jumatatu juma hili, mitihani ya kumaliza kidato cha nne inaendelea nchini kote. Mtihani ni utaratibu uliowekwa kwa ajili ya kuwapima wanafunzi uelewa wa masomo waliyojifunza kwa kipindi fulani.

Jambo la kusikitisha kusikitisha ni kwamba mwanzo si mzuri mwaka huu. Mara kipyenga kilipopulizwa cha kuashiria kuanza kwa mitihani hiyo, tayari mtihani wa hesabu umeshavuja!
Shule za "English Medium" na za kulipia ndiyo hasa zilizobambwa katika mkasa huu-k.m. Happy Skillful! Ni aibu kwa kweli. Ni aibu kwasababu wazazi wamewasomesha watoto wao kwa gharama kubwa lakini hatimaye wanaiba mtihani.

Lakini kwa upande mwingine wazazi nao wanahusika kwa kiasi kikubwakatika kashfa hii. Wanafunzi watapata wapi fedha za kununua mtihani? Pengine tuseme wamiliki wa shule, hasa hizi za kulipia maana wanataka sifa, wanataka kujitangaza kuwa wee-HappySkillful - Mathematics A- 20! Kati ya hao wasichana ni 12! Acha mchezo. Kwanini wazazi wasishawishike kuwapeleka watoto huko na kwa kufanya hivyo - definetily mwenye shule ataongeza karo. Mikakati iwekwe kukomesha mtindo huu vinginevyo watoto wa wanyonge hawataona Kidato cha Tano na huko Chuo Kikuu itakuwa ni ndoto. Hivi kweli tunalipeleka wapi Taifa hili. Ama kweli sitakosea kwa kuliita kuwa ni Taifa la "Vodacom"

No comments: