Thursday, October 9, 2008

WIKI YA NYERERE SIJUI MNAONAJE

Vyombo vya habari vimeanza kuandika sana kuhusu wiki ya Nyerere 13-18 Oktoba.

Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere ndiye Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nyerere ameongoza Taifa hili kwa muda mrefu sana yapata miaka 21 (Tanzania). Kipindi hicho si kidogo ni umri wa mtu mzima +3. Katika kipindi hicho mambo mengi yamepangwa na mengi ambayo yametekelezwa na ambayo hayakutekelezwa.

Wakati yanaandikwa mengi kuhusu Nyerere. Kuna baadhi ya Wataznania wanadai kuwa Nyerere alitupeleka pabaya! Hivi ni kweli? Kama kweli kumbukumbu hii ni ya kinafiki. Mimi namuheshimu sana Mwl. Nyerere na sera zake nazikubali. Watanzania wengi wamefikishwa hapa walipo kutoka na sera zilizokuwepo za elimu, afya na uzalishaji. Sijui wenzangu mnaonaje.

No comments: