Friday, October 24, 2008

Watanzania wameanza kutojiamini

Inavyoonekana kuwa kwa sasa hali ya kujiamini kwa Watanzania inapungua kwa kasi ya kutisha. Hii inajionyesha kwa kuvuja mitihani, majengo kuanguka, mabarabara kujengwa kwa kiwango cha hali ya chini. Wagonjwa kupata tiba isiyowahusu. Kutofanya vizuri kwenye michezo ( olimpiki 2008).

Kama mwanafunzi amehudhuria elimu ya sekondari kwa miaka 4 kwa nini aibe mtihani? (Huko ni kutojiamini). Kama mwanamichezo amefanya mazoezi vizuri na kufuata miiko ya wanamichezo sioni sababu ya kutofanya vizuri.

Kama wahandisi wamepata elimu na uzoefu wa kutosha katika kazi yao kwanini washindwe kusimamia kazi zao za ujenzi.

Watanzania turudishe hali ya kujiamini hata kama tunakosea lakini tunajifunza kutokana na makosa tunakokwenda siko. Watakuja wageni kutufanyia kila kitu kwani hatujiamini na hatuaminiani.

No comments: