Monday, November 3, 2008

Joseph Kamsopi afanya kweli


Kijana mtanashati wa mchanganyiko wa Kimanda kutoka ziwa Nyasa na Kiluguru kutoka Morogoro mji kasoro bahari-Matombo, Kiswira - Joseph Kamsopi Mdimi amefanya kweli baada ya kufunga pingu za maisha na Bi Flora Yesusaa Msechu wa Kilimanjaro.



Harusi hii ilifungwa katika Kanisa Katoliki la Mwenye Heri Anuarite, Makuburi -External - Dar Es Salaam tarehe 18/10/2008 na kisha sherehe ya kufana ilifanyika katika Ukumbi wa Afri-Centre Msimbazi - jijini Dar Es Salaam. Hebu waone maharusi hapo kushoto juu wanapendeza ehee!

No comments: