Thursday, November 13, 2008

Wamisionari wametuachia urithi mkubwa lakini bado tumelala

Wiki ya jana nilisafiri kwenda Morogoro kushiriki katika mazishi ya Binti yetu Rose Aniani Mbiki (Mtoto wa mdogo wangu) aliyefariki pale Bigwa Morogoro. Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu Rose.

Ibada takatifu ya mazishi ya kumuombea marehemu ilifanyika kwenye kanisa la Bigwa (Sekondari ya Masista-Bigwa). Sijawahi kuingia ndani ya Kanisa hilo lakini nilivutiwa sana kwa jinsi Kanisa hilo lilivyojengwa kwa matofali ya kuchoma kwa mpangilio mzuri tu. Milango ilivyotengenezwa inapendeza na utaalamu wa hali juu umetumika.

Makanisa mengi ya jimbo la Morogoro yamejengwa zamani na Wamisionari. Ukiangalia utaalamu uliotumika ni wa hali ya juu sana ukizingatia na hali halisi ya vifaa kwa wakati ule. Bado sielewi, hivi ni kwanini tunashindwa kuuendeleza utaalamu ule? Udongo ni uleule watu wapo kwanini tusiboreshe yale tuliyoyakuta na kusonga mbele? Ajira tunazozitafuta si kama hizi za ujenzi? Vijana wangapi wa Bigwa, Matombo na Morogoro kwa ujumla wamerithi taalama hii ya ujenzi au wanajenga kwa kulipua tu?

No comments: