Thursday, November 13, 2008

Wafanyabiashara ndogondogo waelimishwe

Idadi kubwa ya watu jijini Dar Es Salaam na miji mingine hapa nchini hufanya biashara ndogondogo. Lakini leo hii nitazungumzia biashara za vyakula, matunda na vitafunwa.

Utamkuta mtu anauza korosho, karanga, majibaridi, maembe, pilau, samaki wa kukaanga n.k. Lakini yeye mwenyewe mchafu, chombo alichowekea chakula kichafu, mazingira anayouzia chakula ni machafu. Hivi kweli kwa hali hii mteja anaweza kuvutiwa na biashara yako?

Mimi napenda sana kutafuna korosho, lakini wakati mwingine nasita kununua korosho ambazo zinauzwa na mtoto mdogo mchafu ambaye huchezea chezea korosho hizo wakati akizipanga kwenye mafungu. Au utakuta mwanamama anauza chakula huku ananyonyesha au kujikuna sehemu mbalimbali. Kwa hali hii ni vizuri wafanyabiashara ndogondogo wakaelimishwa. Si elimu ya mikopo tu bali jinsi gani wanavyoweza kuvutia biashara zao.

No comments: