Monday, November 24, 2008

Taxi za njano

Ukitua uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi utakutana na magari mengi sana ya aina mbalimbali na mazuri kwa kusema ukweli. Hata hivyo magari madogo ya abiria yaliyopakwa rangi ya njano yanavutia zaidi hapo uwanjani (Lakini si magari ya Dar Young Africans). Magari hayo ni utambulisho kuwa ni zile Taxi zinazo park uwanjani hapo na ubavuni kuandikwa JKIA. Magari hayo ni masafi yanavutia na yana utaratibu mzuri kwa abiria. Ni vizuri kwa Taxi za zinazo park Dar- Mwl. Julius Nyerere International Airport zikaiga utaratibu huu na kuwa na nauli zakuridhisha kwa wateja na si kuwatega watejawaingizwe king! Kipato hakipatikani kwa ujanja ujanja! Tuwe wastaarabu na tuvute wateja kwa mambo mazuri.

No comments: