Friday, November 14, 2008

Viongozi wa nchi wavalia njuga kilimo na kuona kuwa inawezekana

Viongozi wetu wengi wameanza kuhamasisha na kufuatilia shughuli za uzalishaji wa kilimo kwa vitendo na sasa inaonekana kuwa kila kitu kinawezekana kwa ajili ya kuendeleza Kilimo.


Hivi majuzi tu Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda katika ziara yake mkoani Dodoma aliweka mkwara mkali kwa wakuu wa wilaya na mikoa kwamba wakati wa kuvaa suti kila siku umekwisha wanahitajika kuvalia njuga kilimo kwa nguvu zao zote.


Tayari Mkuu wa wilaya ya Kondoa Bw Seif Mpembenwe amemweleza Waziri Mkuu kuwa wilaya yake inaweza kujitosheleza kwa chakula. Sasa kama wilaya zote zitaahidi hivyo na kukipa kilimo kipaumbele katika shughuli zake, tatizo liko wapi?

No comments: