Friday, November 14, 2008

Hongera wanamichezo wa "KILIMO"

Timu ya michezo ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika mwaka huu 2008 imefanya maajabu kule Morogoro kwenye mashindano ya SHIMIWI. Wameweza kuwa washindi wa jumla wa tatu kati ya timu 54 zilizoshiriki.

Kilimo imeweza kuwa mshindi wa tatu katika mpira wa Miguu, mshindi wa nne mpira wa pete, bao mshindi wa pili na riadha wamepata medali. Hii imetokana na maandalizi mazuri, kujituma na nidhamu ya hali ya juu waliokuwa nayo wachezaji wakati wote wamaandalizi na mashindano. Hongera sana Mwenyekiti wa Kilimo Sports Klabu Bw. George Mbelwa.

No comments: