Thursday, November 13, 2008

Wafanyakazi wa Kilimo watakiwa kufanya Kazi kwa taaluma

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara hiyo Bw Peniel Lyimo, ametoa agizo kwa wafanyakazi wote wa wizara yake kufanya kazi kwa kuzingatia taaluma zao walizoajiriwa ili kuboresha utendaji wa kazi.
Akitoa mfano alisema kuwa si vizuri kwa Mkufunzi kufanya kazi za Mhasibu au Mhasibu kufanya kazi za ugavi. Alisisitiza kwa kusema kuwa kazi zote zinafanywa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu kulingana na taaluma.

Mwenyekiti huyo alitoa agizo hilo wakati wa kikao cha Baraza kilichofanyika tarehe 8/11/2008 mjini Morogoro katika Ukumbi wa Morogoro Hotel na kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali wa Baraza hilo wakiwemo Wakurugenzi, Wakurugenzi wa Kanda, Wawakilishi kutoka Vyama Vya Wafanyakazi (TUGHE & RAAWU) na Wawakilishi wa Wafanyakazi.

No comments: