Friday, November 14, 2008

Machungwa yako sokoni

Watanzania sasa tunaanza kufaidi matokeo ya teknolojia bora za kilimo. Machungwa sasa yanapatikana sokoni wakati huu mwezi Novemba tena matamu sana, tena makubwa na tena kwa bei poa.

Iwapo sekta ya kilimo itaongezewa raslimali kwa asilimia 5 tu , kile kisichowezekana kitawezekana na kuwa na ziada. Mazao mengi yanayoonekana sokoni hivi sasa ni juhudi za mkulima huyu mdogomdogo, asiyekuwa na pembejeo bora za kilimo, anayetumia zana duni za kilimo na anayetegemea kilimo cha mvua!

No comments: