Monday, November 24, 2008

Huduma za Hotelini Kenya ni zaidi

Ukiwa Hotelini Nairobi Kenya, huduma nyingi zinapatikana ikiwamo hii ya Internet. Hapa nilipo nimeweza kuwasiliana nanyi kwa kutumia "Wireless internet connection" huna haja ya kuonana na mtu anayekupa hiyo huduma. Upo chumbani kwako unapiga simu na unapata huduma kwa maelekezo.Malipo baadaye na ni malipo nafuu.

Hee, hata kama mimi ni mtalii ningeweza kupendelea kwenda Kenya. Hivi vitu vinawezekana kwetu pia. Nafahamu huduma hizi zipo kwetu lakini hazijaenea kwa kiasi cha kutosha lakini inawezekana. Tunapoteza hela nyingi kwenye sekta ya mawasiliano tumeng'ang'ania simu za mkononi tu. Wenzetu wanahama taratibu!

No comments: