Monday, November 24, 2008

Kweli inawezekana watoto wasiwe wa kwako

Nipo hapa Intercontinental Hotel Nairobi, Kenya. Nimekutana na wasomi kutoka Kenya, Uganda, Eriteria, Burundi na Rwanda. Siku ya leo tumezungumzia sana kuhusu kilichotuleta hapa Kenya hasa kuhusu masuala ya "Kupelemba na Kutathmini "( Monitoring and Evaluation)shughuli za Utafiti, Ugani na Mafunzo katika eneo hili la Afrika ya Mashariki na ya Kati.

Mazungumzo nje ya hilo yanagusa masuala mbalimbali.Lakini kwa kuwa ni watu wazima na tupo jinsi mbili tunazungumza yanayotuhusu katika maisha yetu ya kila siku. Katika hilo lililochukua muda mwingi ni mahusiano ya ndoa. Imebainika kuwa mwanamke anaweza kubeba siri kubwa kuhusu baba halisi wa watoto. Je hili mnalionaje wana mtandao?

No comments: