Thursday, November 13, 2008

Sababu za foleni barabara ya Kilwa

Barabara ya Kilwa ninaitumia karibu kila siku. Kwa sasa barabara hiyo iko kwenye ukarabati mkubwa. Barabara inapanuliwa na madaraja mapya yanajengwa. Kutokana na hali hiyo huwa kunatokea usumbufu mkubwa wa usafiri wakati wa asubuhi na jioni. Safari ya dkika ishirini inaweza kuchukua zaidi ya saa moja. Sababu kubwa ya kuwa na foleni yakukatisha tamaa hata kusababisha watu wengi kutembea kwa miguu ni hizi hapa.

  • Madereva wasiozingatia sheria na taratibu za kuendesha magari
  • Wajenzi wa barabara kutoweka vizuizi kwa sehemu ambazo hazistahili kupita magari
  • Askari wa Usalama barabarani (Traffic Police) kutofanya kazi yao barabara kwa kuelekeza za kupita magari.
  • Viongozi wa Manispaa ya Temeke kutolishughulikia suala hili ili liweze kupatiwa ufumbuzi wa muda wakati barabara hiyo inajengwa.

No comments: