Monday, November 24, 2008

Nikiwa Kenya niko Nyumbani

Nairobi, watu wake, miti yake na udongo wake ni kama Arusha tu. Isitoshe Wakenya wanaongea na kukipenda Kiswahili tofauti na jinsi Watanzania wengi wanavyohisi kuhusu Wakenya. Kwa kweli ukiwa Kenya unajisikia nyumbani. Utasikia watu wanakusalimia habari mzee. Wanasema yule "demu" ameondoka. Wanakuambia bia baridi ndiyo yenyewe. Wageni wengi wangependa kufahamu na kuzungumza Kiswahili wakiwa Kenya. Watanzania mpo?

No comments: