Monday, November 24, 2008

Watanzania tulishapita hatua ya Waamerika

Niko hapa Nairobi Kenya, nimetoka kwenye "reception dinner" iliyoandaliwa na wenyeji wetu ASARECA kwenye warsha hii ya "Kupelemba na Kutathmini" miradi ya ASARECA.



Kwa faida ya wale ambao hawaifahamu ASARECA. Huu ni chombo cha Afrika mashariki na Kati kinachoangalia masuala ya Utafiti, Ugani na Mafunzo Katika Kilimo.



Ndugu zangu wa Kenya wamekiri kuwa hakuna cha kushangaza kuhusu Obama kuwa Rais wa Amerika. Watanzania wameshapita hatua hiyo siku nyingi. Wanaeleza wenyewe kuwa kwa Tanzania hawakuwa na sababu ya kufahamu kuwa Mkapa alikuwa anatoka wapi. Walichotaka ni kuwa na Rais atakayeweza kuisimamia nchi ya Tanzania. Watanzania tupige makofi basi kuwa tunawazidi hata Waamerika kwa hilo. Lakini kwa nini hatupigi hatu kwenye Maendeleo?

No comments: