Friday, November 14, 2008

Habari na Mawasiliano ni nyenzo muhimu katika Kilimo

Mwezi Septemba mwaka 2008 nilibahatika kuhudhuria warsha ya wadau wa habari na mawasiliano katika sekta ya Kilimo kutoka nchi za SADC iliyofanyika nchini Botswana, jijini Gaborone.

Nchi 14 ukiondoa Afrika ya Kusini zilishiriki warsha hiyo iliyokuwa na dhumuni la kuona jinsi gani nchi za SADC zinavyoweza kuwasiliana na kutumia tekenoljia ya habari, katika masuala mbalimbali ya kilimo kwa kutumia vyombo mbalimbali kwa kuzingatia wadau.

Wakati umefika sasa wa kukitangaza kilimo kama vile inavyotangazwa " cocacola" lakini mawasiliano hayo ni vyema yakawaongezea maarifa wadau wetu wa kilimo. Tunataka kilimo chenye kumnufaisha mkulima.

Kuna mambo mazuri yanayofanyika katika nchi hizi ambazo yanawezwa kuigwa na nchi nyingine lakini hayafahamiki. Kuna matukio muhimu yanayotokea katika sekta ya kilimo lakini yanabakia palepale. Basi ilionekana kuwa kuna umuhimu wa kila nchi kuangalia jinsi ya kutumia taarifa, mawasiliano na teknolojia ya habari katika kuboresha sekta hii.

Wakati viongozi wetu wanapiga kelele na kuhamasisha uzalishaji katika kilimo, habari na mawasiliano ni nyenzo muhimu itakayosaidia kuboresha kilimo chetu. Pichani wanaonekana washiriki wa warasha hiyo.

No comments: