Thursday, November 13, 2008

Keep Left hiki cha Kituo cha Polisi Chang'ombe

Imenipasa kuandika kuhusu "Keepleft" kilichojengwa katika makutano ya barabara ya Sokota na na Chang'ombe karibu kabisa na Kituo cha Polisi Chang'ombe na Kanisa Katoliki Parokia ya Chang'ombe hapa jijini Dar Es Salaam.

Ukarabati wa barabara wa mahali hapo ambapo hapo awali palikuwa korofi sana sasa umekamilika na kipya kilichoongezwa ni kujengwa "Keepleft" asante sana. Lakini tangu kijengwe "Keepleft" hicho hakuona lolote la zaidi. Maua hayajapandwa.Kwa kifupi "Keepleft" hicho hakivutii kabisa sijui ni jukumu la nani. Manisapaa ya Temeke? TANROADS au nani ?Tuelewesheni basi.

No comments: