Friday, November 14, 2008

Kanisa Katoliki Parokia ya Vikindu -Mt. Vincent wa Paulo



Hili ndilo Kanisa ninalosali mimi. Kanisa Katoliki la Parokia ya Vikindu. Kanisa hili tumelijenga kwa nguvu zetu sisi waumini pamoja na marafiki zetu wa ndani na nje ya nchi. Kanisa hili limejengwa na baadhi ya waislamu waliojitolea bila kujali tofauti ya dini.Ndiyo hatukumsubiri OBAMA.Tulijtegemea wenyewe.

Nilipohamia Vikindu-Kisemvule mwaka 2004, tulikuwa tunasali kwenye ukumbi mdogo tu. waumini tulikuwa wachache sana hata sadaka ilikuwa chache pia. Ibada Takatifu siku ya Jumapili ilikuwa ni moja sasa kuna misa ya pili ya watoto. Kanisa hili zuri lina vipaaza sauti, lina madawati mazuri ya kukalia, lina kwaya nzuri pia na kwa kweli linapendeza ndani na nje. Karibuni sana Vikindu.
Parokiani Vikindu kuna Zahanati nzuri tu, kuna shule ya watoto wadogo na shule ya msingi ambayo hufundisha kwa kiingereza zote zinamilikwa na Parokia ya Vikindu. Kanisa limeleta maendeleo ya kiroho na kimwili. Watawa wa Vikindu wanapaita mahali hapo "Jesus Town"

No comments: