Tuesday, November 25, 2008

Utekelezaji mbovu Afrika ndo unaotufanya tusifikie malengo

Jana katika hotel ya Intercontinental hapa Nairobi, Kenya tulikuwa tunajadili masuala ya "kupelemba na kutathmini" (Monitoring and Evaluation) kwenye utafiti wa Kilimo.

Imedhihirika kuwa tuna mipango mizuri yenye malengo mazuri. Na malengo yetu makuu kwnye nchi hizi za Afrika Mashariki na ya Kati kwa bahati nzuri ni ya muda mrefu sana kama vile kuondoa umaskini, ujinga, maradhi lakini hadi hii leo tunazungumzia hayo hayo tokea tupate UHURU. Korea ya Kusini walikuwa kwenye hali kama yetu miaka 40 iliyopita sasa wameshatoka. India sasa wanajitosheleza kwa chakula! Sisi misaada, misaada misaada!

No comments: