Friday, December 5, 2008

Unapokutana na mfugaji kutoka Twatwatwa ukiwa Nairobi

Adam Ole Mwarabu ni mfugaji kutoka kijiji cha Twatwa, Kilosa, Morogoro. Kijiji hiki ni maarufu kwa mapigano kati ya Wafugaji (Wamasai) na wakulima. Adam ni Mmasai. Hivi karibuni nilikutana na Adamu uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JomoKenyatta Jijini Nairobi wakati tukisubiri ndege ya kurudi nyumbani Tanzania (Dar Es Salaam). Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kukutana na Adam. Huku akivalia lubega na kubeba "laptop" yake ni lazima utajiuliza kimoyomoyo hivi Mmasai anaweza kutumia Laptop?

Adam, ni Mmasai aliyendelea. Amesafiri nchi nyingi hapa duniani kuliko wengi wetu. Amehudhuria mikutano mingi ya kimataifa na wakati nilipokutana naye alikuwa anatokea Ubalozi wa Poland kuchukua Visa.

Adam ni Mratibu wa NGO inayooitwa PAKODEO (nitamuuliza kirefu chake). NGO hii hujishughulisha zaidi na masuala ya ardhi, mifugo, elimu, mazingira na jinsi ya kupambana na HIV-AIDS.

Adam hazungumzii zaidi kuhusu mapigano ya wakulima na wafugaji anasema ni ya kisiasa zaidi na viongozi hawako makini katika kutatua tatizo.

No comments: