Wednesday, December 31, 2008

Kwaheri 2008

Kwaheri 2008.

Mwaka huu ulikuwa wamafanikio makubwa kwa blog hii. Banzi wa Moro ameweza kuvuka lengo alilojiwekea kwa asilimia 140! Kumbe inawezekana.

Sina budi nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya na busara ya kuweza kukusanya habari mbalimbali na kuweza kuzining'iniza kwenye blog hii.

Nawashukuru viongozi wangu wa kazi walioniwezesha kupata safari za kikazi ndani na nje ya nchi kwazo nimepata fursa ya kuona mengi na kuyaweka ndani ya blog hii.

Kasoro kubwa iliyojitokeza kwa mwaka uliopita ni kwa wasomaji wangu kushindwa kutoa maoni yao kwa habari ambazo zililenga maeneo yenye uzoefu nao.

Ombi langu kwa wasomaji wa blog hii wajitahidi zaidi kutoa maoni yao mwaka ujao. Hii itanipa moyo wa kuweza kukusanya habari nyingi na kuzining'iniza blogini.

Mungu akipenda mwakani naweza kuwa na camera hivyo kuboresha zaidi habari katika blog hii. Mwaka huu mara chache niliweza kudowea camera na kupiga picha chache sana.

Namshukuru mdogo wangu Freddy Mloka, Dada Meab Mdimi ambao wamekuwa wakinitumia picha hasa za familia.

No comments: