Monday, December 29, 2008

Matombo imeanza kupoteza umaarufu wa machungwa matamu

Miaka 20 iliyopita Matombo ilikuwa maarufu sana kwa uzalishaji wa machungwa matamu. Machungwa haya yalijulikana kwa jina la Machungwa ya Matombo. Yalikuwa matamu sana hata rangi yake ilikuwa ya kuvutia mlaji.

Ni kweli miaka hiyo hakukuwa na biashara nzuri ya matunda haya. Nakumbuka babu yangu alikuwa na miti michache ambayo aliweza kuikodisha kwa walimu wa shule ya msingi Matombo kwa bei ya sh 2 kwa mchungwa! Sasa hali hii haipo tena. Uzalishaji umepungua sana na mahitaji yameongezeka sana kiasi cha kuwafanya wafanyabiashara (walanguzi) kuvuna machungwa wakati hayajapata rangi yake nzuri ya njano! Bei ya chungwa moja kwa sasa haitofautiani sana na ile ya Dar Es Salaam.

Miti mingi ya machungwa imeanza kuzeeka au kushambuliwa na wadudu na magonjwa na sikuona jitihada za makusudi kuokoa hali hiyo kwa wakulima wa machungwa. Ndiyo maana nathubutu kusema kuwa Matombo imeanza kupoteza umaarufu wa machungwa matamu.

No comments: