Tuesday, December 23, 2008

Safarini Matombo-Morogoro

Xmass na mwaka mpya unakaribia. Sisi hatuna utaratibu wa kurudi kwetu wakati wa Xmass kama ilivyo kwa wenzetu Wachagga. Hivi sasa huko migombani ni nyimbo za marehemu Jim Reeves tu na harufu ya mbege kumbe je!

Mwaka huu nimeamua kwenda kusherehekea Xmass na ndugu zangu huko kwetu Matombo, nikale Magimbi, Ndizi, mananasi, "ubwabwa na kuku." Nitasafiri kwenda Matombo Morogoro kwa Bibi na Babu zangu, Baba na Mama zangu, Shangazi na Wajomba zangu, Kaka na dada zangu na wengineo.

Nategemea nitaonana na marafiki zangu tuolisoma shule moja, kusali pamoja pale Matombo Mission, kucheza mpira pamoja -Kiswira Sports Club! Nategemea kuimba GLORIA! siku ya Xmass ndani ya Kanisa la Mtakatifu Paul.

Nitakaporudi nitakuwa na mengi ya kuning'iniza kwenye blog hii.

KWAHERINI

No comments: