Wednesday, December 31, 2008

Wamefaulu madarasa hakuna

Matokeo ya mtihani wa darasa la saba yametangazwa lakini kwa bahati mbaya kuna baadhi ya matokeo ya wanafunzi hayajatolewa rasmi eti kwasababu shule zinazotakiwa kuchukuwa wanafunzi hao hazina madarasa! Hali hii imejitokeza zaidi katika mkoa wa Morogoro. Wanafunzi wamefaulu madarasa hakuna.

Sasa viongozi ndo wanakimbizana kutafuta suluhu madarasa yajengwe.
Juzi diwani wa kata ya Mtombozi alifika ofisini kwangu kueleza shida kama hiyo kwa Sekondari ya Mtombizi iliyopo Matombo Morogoro. Jana jioni baadhi yetu tulikutana kujaribu kuweka mikakati ya kuweza kuinasua Mtombozi Sekondari.

Tulichokiona ni kuwa uongozi katika ngazi zote za utekelezaji hauna muono, hauna mikakati. Iweje leo matokeo yanatoka ndo wanakumbuka kujenga madarasa. Hivi jamani Morogoro tuna nini? Hii si lawama kwetu tuonekane hatujali nyumbani?

Hata hivyo tumekubaliana kusaidia kutatua tatizo hilo kwa mikakati tutakayoiweka. Mojawapo ni kuwa na mtandao wa wadau. Na tayari hatua zimeshaanza kuchukuliwa. Hata hivyo tumekubaliana kuwa uongozi uelezwe wazi udhaifu wao. "Wotugwisa"

No comments: